Twahir Sudy
Chief Executive Officer
Mkurugenzi Mkuu
Founder & visionary behind Simamia App. Passionate about building tools that empower small businesses across Tanzania.
Kuziwezesha Biashara za Kitanzania
Kutoka kwenye madaftari hadi kidijitali โ kusaidia biashara ndogo na za kati kusimamia shughuli zao kwa urahisi, bila uhitaji wa intaneti mara kwa mara, ikiwa imetengenezwa mahususi kwa ajili ya Tanzania.
Simamia App ilizaliwa baada ya kuona changamoto halisi wanazokutana nazo wafanyabiashara wadogo na wa kati katika kusimamia mauzo, hesabu za bidhaa, na mtiririko wa pesa kila siku. Tulitaka kuondoa madaftari na mifumo migumu ya kizamani.
Muanzilishi wetu, ambaye ni Mtengenezaji wa Mifumo (Programmer), aliingia mtaani na kufanya biashara mwenyewe kwa zaidi ya miezi saba. Kupitia uzoefu huo wa ndani, alizikabili changamoto halisi za kila siku, kuanzia upotevu wa bidhaa hadi hesabu zisizoeleweka. Uzoefu huo ndio uliomwezesha kutengeneza mfumo halisi na madhubuti unaojibu shida halisi za mfanyabiashara, na si nadharia tu.
Leo, Simamia App imekuwa zaidi ya mfumo wa usimamizi; ni mshirika wa ukuaji kwa mamia ya biashara. Tunaendelea kubuni mbinu mpya za kiteknolojia ili kurahisisha uendeshaji wa biashara kote nchini, kumpa mmiliki udhibiti kamili, na kukuza uchumi wa kidijitali.

Tazama jinsi tulivyotoka kwenye wazo la kawaida na kuwa suluhisho kamili linaloaminika kiganjani mwako.
Hapa ndipo cheche ya kwanza ya Simamia App ilipowaka. Baada ya kuona changamoto za mtaani, wazo rasmi la kutengeneza mfumo thabiti wa usimamizi wa biashara lilizaliwa rasmi.
Hapa ndipo cheche ya kwanza ya Simamia App ilipowaka. Baada ya kuona changamoto za mtaani, wazo rasmi la kutengeneza mfumo thabiti wa usimamizi wa biashara lilizaliwa rasmi.
Tulizindua Landing Page yetu ya kwanza na kukata domain rasmi. Hii ilikuwa hatua muhimu ya kuweka alama yetu ya kwanza mtandaoni na kuanza kukusanya maoni ya awali.
Toleo la kwanza kabisa la mfumo (Beta testing APK) lilizaliwa rasmi. Tulianza majaribio ya ndani kwa ndani na wafanyabiashara wachache ili kuona jinsi mfumo unavyofanya kazi mtaani.
Toleo la kwanza kabisa la mfumo (Beta testing APK) lilizaliwa rasmi. Tulianza majaribio ya ndani kwa ndani na wafanyabiashara wachache ili kuona jinsi mfumo unavyofanya kazi mtaani.
Baada ya kupokea mrejesho kutoka kwenye majaribio ya awali, tulizindua toleo la v1.1.2 lililokuwa na kasi zaidi, usalama wa juu wa data, na muonekano rahisi zaidi kutumia.
Hatua kubwa ya mafanikio! Simamia App sasa inapatikana rasmi Google Play Store. Kila mfanyabiashara anaweza kuipakua kwa urahisi na kuanza kuongoza biashara yake kidijitali.
Hatua kubwa ya mafanikio! Simamia App sasa inapatikana rasmi Google Play Store. Kila mfanyabiashara anaweza kuipakua kwa urahisi na kuanza kuongoza biashara yake kidijitali.
Kusaidia biashara ndogo na za kati Tanzania kusimamia shughuli zao bila msongo wa mawazo na kwa urahisi โ kubadilika kutoka matumizi ya vitabu vya kawaida kwenda kwenye suluhisho rahisi za kidijitali.
Wazo lilikuja wakati wa kufuatilia mauzo, matumizi, na faida katika duka la nyumbani huko Arusha, Tanzania. Tuliona hitaji la suluhisho rahisi linalofanya kazi hata bila intaneti na linaloendana na biashara halisi za Tanzania.
Maduka Madogo
Rejareja na Huduma
Mini Market
Supermarket
Hakuna POS Inayohitajika
Simu Yako Inatosha
Fuatilia Kila Kitu
Mauzo na Faida
Imeundwa mahususi kwa ajili ya mazingira ya biashara ya Kitanzania
Rekodi mauzo, angalia data zako, na fanya kila kitu bila uhitaji wa intaneti kwa muda mrefu. Ni mfumo mzuri kwa maeneo yenye mtandao usio imara. Data zako zitasawazishwa kiotomatiki ukiunganishwa tena.
Hakuna kurudia kuandika kila wakati. Weka mauzo mapya kwa urahisi kabisa. Mfumo wetu wa kijanja unakumbuka bidhaa na wateja wako, na kufanya kila mauzo kuwa ya haraka zaidi kuliko ya awali.
Timu ndogo yenye moyo mkubwa โ inayojitolea kuwapa wafanyabiashara wadogo zana za kisasa za kusimamia biashara zao.
Chief Executive Officer
Mkurugenzi Mkuu
Founder & visionary behind Simamia App. Passionate about building tools that empower small businesses across Tanzania.
Chief Sponsor
Mdhamini Mkuu
The backbone of our mission. Providing strategic guidance and unwavering support to help Simamia grow and reach more merchants.
Market Agent
Wakala wa Masoko
Connecting Simamia App with merchants on the ground. Ensuring every shop, kiosk, and duka gets the tools they need to thrive.
Simamia App โ Simamia mauzo, fuatilia madeni, na angalia faida zako moja kwa moja kutoka kwenye simu yako, bila daftari wala mahesabu.
Simamia biashara yako popote ulipo.
Angalia faida zako kwa kubonyeza tu.
Hakuna mahesabu ya mkono tena.
"Sikuwa najua madeni yangu yalikuwa mangapi. Simamia imenionesha kwa sekunde โ sasa napata faida yangu halisi kila siku!"
Mama Rehema
Duka la Nafaka ยท Dar es Salaam
"Nilikuwa na daftari nyingi zilizopotea. Sasa mauzo yote, madeni, na faida โ yote kwenye simu yangu. Ni rahisi sana!"
Juma Hassan
Mini Market ยท Zanzibar
"Wateja wangu wanadai, lakini sasa Simamia inakumbusha kila deni. Biashara yangu imekua kwa 40% ndani ya miezi mitatu!"
Amina Mwinyi
Duka la Nguo ยท Arusha
Bure ยท Rahisi ยท Salama
Timu yetu ya usaidizi iko tayari kukusaidia. Tupigie simu, tutumie ujumbe WhatsApp, au tembelea ofisi yetu Dar es Salaam.