1. Taarifa Tunazokusanya
Ili kukupatia huduma bora kupitia Simamia App, tunakusanya taarifa zifuatazo kulingana na matumizi yako:
- Taarifa za Akaunti: Barua pepe (email), namba ya simu, na jina la biashara yako wakati wa usajili au uthibitisho wa OTP.
- Guest Mode: Ukitumia app kama mgeni bila akaunti, taarifa zako huhifadhiwa ndani ya kifaa chako pekee.
- Data za Biashara: Bidhaa, stock, mauzo, matumizi (expenses), faida, madeni, na oda.
- Taarifa za Wateja: Namba za simu au taarifa unazoingiza kwa ajili ya oda, WhatsApp, au SMS.
2. Jinsi Tunavyotumia Taarifa Zako
Taarifa zako hutumika kwa madhumuni yafuatayo pekee:
- Kufuatilia mwenendo wa biashara yako kupitia ripoti, historia ya mauzo, na faida.
- Kusindika oda, kubadili hali ya malipo, na kurahisisha mawasiliano na wateja.
- Kuhakiki malipo ya vifurushi kupitia Transaction ID.
- Kuboresha utendaji wa app na kuhifadhi mipangilio yako ya mwisho.
3. Uhifadhi na Ulinzi wa Data
Tunachukua hatua mbalimbali kuhakikisha data zako zinalindwa kwa usalama mkubwa.
Udhibiti wa Data: Unaweza kufanya Export DB au Import DB kupitia sehemu ya Settings ili kulinda taarifa zako.
Kufuta Data: Ukichagua “Futa Data Zote”, taarifa zako zote zitafutwa kabisa na hatua hiyo haiwezi kurejeshwa.
4. Ruhusa za Kifaa
Simamia App inaweza kuomba ruhusa zifuatazo ili vipengele vya mfumo vifanye kazi vizuri:
- Kamera/Scanner: Kukagua barcode za bidhaa.
- Storage: Kupakua PDF, CSV, na kufanya bulk import ya bidhaa.
- Simu & Mawasiliano: Kupiga simu au kutuma WhatsApp/SMS moja kwa moja kwa wateja.
5. Mabadiliko ya Sera Hii
Tunaweza kuboresha sera hii mara kwa mara ili kuendana na mabadiliko ya sheria au maboresho ya vipengele vipya vya Simamia App.
6. Wasiliana Nasi
Kama una maswali, maoni, au unahitaji msaada kuhusu sera hii ya faragha, unaweza kuwasiliana nasi kupitia:
Simu: +255 798 700 900
Msaada: Angalia video za mwongozo ndani ya app.